Posts

Showing posts from May, 2020

FAHAMU NAMNA NZURI YA KUVUNA MAJI YA MVUA KWA AJILI YA KILIMO NA MIFUGO

Image
  Katika maeneo mengi ya Afrika mashariki hususani Tanzania tuna kiasi  kikubwa sana cha maji kwenye mito, chemichemi, maziwa na maji ya ardhini(undergroundwater) ambapo asilimia 70% hutumika kwenye kilimo kwa kuzalisha mazao mbalimbali Lakini kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na tabia ya nchi mvua iliyokuwa ikitegemewa sana na wakulima kama chanzo cha maji kwa mimea imekuwa sio ya kuaminika tena kwani hainyeshi tena kwa wakati, hunyesha kwa kiasi kidogo sana(450mm-600mm), maeneo mengine hunyesha kwa kiasi kikubwa sana mpaka kusababisha mafuriko ambayo huharibu vibaya mazao ya wakulima mashambani, pia baadhi ya vyanzo vya maji vimekauka na hivyo kusababisha uhaba mkubwa sana wa maji sio tuu kwenye kilimo bali hata kwenye upatinaji wa maji safi kwa matumizi ya nyumbani KWA NINI TUVUNE MAJI YA MVUA Kama nilipoeleza hapo awali kuwa kuna baadhi ya maeneo mvua hunyesha kwa kiasi kidogo sana na hivyo hazitoshelezi kumalizia msimu mzima ili...

AINA ZA UDONGO ZINAZOPATIAKANA TANZANIA

Image
  Udongo ni rasilimali muhimu inayotumiwa katika shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo ambacho kinategemewa na watanzania kuendesha uchumi wa taifa. Lakini uharibifu wa mazingira umechangia kushuka kwa thamani ya ardhi na kuathiri kilimo cha mazao, mifugo na uvuvi. Kutokana na mabadiliko yanayojitokeza kwenye udongo, wananchi wameshauriwa kulima mazao yanayoendana na aina ya udongo uliopo katika eneo husika. Tanzania ni moja lakini udongo hutofautiana kutoka eneo moja hadi lingine ambapo mazao yanayolimwa hutofautiana katika eneo husika ili kuhakikisha uwiano mzuri wa mazao yanayolimwa nchini. Aina za Udongo zinazopatikana nchini Udongo wa kichanga Ukanda wa Pwani ambao unajumuisha mikoa ya Dar es salaam na Pwani, sehemu kubwa ya udongo wake ni ya kichanga.  Udongo wa kichanga huundwa kutokana na kuvunjika vunjika na kumomonyoka kwa miamba kama vile mawe ya chokaa, matale, mawe meupe ya kung’aa na mwambatope. Udongo huu hauhifadhi maji ambapo maji ...

FAHAMU KUHUSU UFUGAJI WA KUKU WEUSI KUTOKA MALAWI (AUSTRALORP)

Image
  Australorp wanastahimili mazingira tofauti, kama kuku wa kienyeji aliye zoeleka nchini Tanzania. Na ni wazuri kwa ufugaji huria, kwa kuwaachia nje wajitafutie chakula wenyewe. Ingawa wanajulikana kwa sifa yao ya utagaji mayai mengi, lakini kuku hawa wanafaa kwa nyama pia, kwani huwa na nyama nyingi sana (dual purpose chickens) Kuku hawa huweza kumpatia mfugaji faida kubwa, kwani ni wazuri kwa biashara ya mayai na nyama pia. Hawana sifa nzuri ya kulalia mayai, lakini akilalia hutotoa vifaranga vingi, na ni wazuri kwa uleaji wa vifaranga hivyo. Utagaji wao wa mayai unakaribia ule wa kuku wa kizungu. Kuku hawa ni wakubwa, wazito, na wanamvuto sana kuwaangalia. Wanapendeza pia kwa ufugaji mdogo, katika mazingira ya nyumbani. Wana michirizi ya kijani pale wanapomulikwa kwenye mwanga mkali wa jua. Kwa wastani Black Australorp, hufikisha mayai 250 kwa mwaka, wakiwa katika mazimgira mazuri. Kuku hawa ni wapole na rafiki kwa binadamu. Black Australorp ni wagumu, ha...

MISINGI YA KILIOMO BORA CHA KAROTI

Image
  Karoti ni zao la mbogamboga ambalo ni zao mzizi, kwa kawaida hupatikana katika rangi ya machungwa,  nyekundu, njano. Karoti za sasa zimetokeza kutokana na karoti pori, Daucus carota. Karoti hutumika sana kwaajili ya kuongeza radha kama kiungo kwenye mboga au kwenye kachumbari na pia zinafaida kubwa katika mwili kwa kukupatia vitamin A na C pamoja na madini ya chuma hasa pale mtu atafunapo. Hali ya hewa na udongo. Karoti zinahitaji hali isiyokuwa na joto sana, wala baridi sana, kati ya nyuzi za degree 15 mpaka 27 za sentigredi. Kama ukanda wa pwani una joto kali, inatakiwa karoti zilimwa miezi ya majira ya baridi, karoti zinazotoka mazingira ya baridi huwa na radha nzuri pamoja na harufu nzuri. Udongo wa kichanga chepesi na tifutifu ndio unafaa katika kilimo cha karoti, udongo wa mfinyanzi na udongo mzito hudumaza mazao. Utayarisha wa shamba. Karoti zinahitaji Shamba la Karoti lilimwe kwa trekta, kwa ng’ombe ama kwa jembe la mkono kwa kina cha sen...